May 9, 2013



Kocha Mkuu wa zamani wa timu ya taifa ya Afrika Kusini, Pitso Mosimane ameshangazwa kusikia kiungo wa zamani wa Simba, Selemani Matola hadi leo hana timu anayoifundisha.

Mosimane aliyewahi kuwa kocha mkuu wa Supersport United, ameiambia Salehjembe ambakuwa akitaka kujua kuhusiana na Matola ambaye anaamini ni kati ya viungo bora aliowahi kuwaona.


“Mchezaji akiwa na uwezo wa kuiongoza timu uwanjani wakati akicheza, ujue ana nafasi kubwa ya kuwa kocha bora.

“Tokea akiwa anacheza chini yangu, niliamini Matola angekuja kuwa kocha bora kabisa. Lakini kama sasa hana timu, huenda hapendi kufanya kazi ya ukocha,” alisema Mosimane kutoka Afrika Kusini.

“Niliwahi kumuambia, unajua wakati anacheza kwamba anaweza kuwa kocha, anajua kubadilisha mpira na wakati gani afanye hivyo na timu icheze,” alisema Mosimane.

Wakati akiwa kocha Supersport, Mosimane alimsajili Matola hata bila ya kumfanyia majaribio baada ya kuiongoza Simba kutwaa Kombe la Tusker jijini Nairobi kwa kuifunga timu yake bao 1-0 na Hearts of Oak kwa mabao 4-2.


Matola alikuwa kocha wa timu ya vijana ya Simba aliyoisaidia kufanya vizuri ikiwa ni pamoja na kutwaa Kombe la BancABC.
Lakini baadaye alikorofishana na uongozi wa Simba chini ya Ismail Aden Rage na kuamua kuachia ngazi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic