May 11, 2013




Kocha mwenye vituko, Jose Mourinho amewaambia waandishi wa habari wa shirika la Sky Sports la Uingereza kwamba Alex Ferguson ni rafiki yake mkubwa na anajua atakwenda timu gani baada ya kuondoka Real Madrid.

Mourinho raia wa Ureno amesema alikutana na Ferguson na akamueleza kwamba atastaafu kitu kilichomshitua sana na alikuwa kati ya watu waliojua mapema suala hilo.

“Ulikuwa ukienda kucheza Old Trafford unaanza kumfikiria Ferguson kuliko timu utakayocheza nayo, aliponiambia nilishtuka sana. Hakikuwa kitu kilichokifikiria na ilinichukua muda kuamini.


“Yeye pia anajua baada ya Madrid nitakwenda wapi, tunabadilishana mawazo kuhusu mambo mengi tu kwa kuwa sisi ni marafiki wa karibu.

“Kuhusu Moyes, nafikiri ni mtu sahihi kabisa na atapata mafanikio makubwa akiwa na Real Madrid. Mambo mengi anafanana na Ferguson na kazi yake ni nzuri, muda utatoa majibu lakini vizuri wakamuamini.

“Uamuzi wa Ferguson umekuwa ni sahihi na katika wakati mwafaka na anastahili kula maisha kwa utulivu kwa kuwa amefanya kazi kubwa,” alifunguka Mourinho.

Awali kulikuwa na taarifa Mourinho angepewa kazi ya kuinoa Manchester United baada ya Ferguson kutangaza kustaafu mwishoni mwa msimu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic