May 23, 2013




Rais wa zamani wa Real Madrid, Ramon Calderon ameanzisha mjadala mpya baada ya kusema mshambuliaji nyota wa timu hiyo, Cristiano Ronaldo ana nafasi kubwa ya kumfuata kocha wake wa sasa Jose Mourinho atakapojiunga na Chelsea.

Tayari Mourinho amethibishwa kuwa atajiunga na Chelsea na Ronaldo amekuwa kati ya wachezaji anaowataka kuungana nao na kufanya nao kazi pamoja.

Ronaldo, 27, imeelezwa dau lake linabaki kuwa pauni milioni 80, fedha walizolipa Real Madrid kumchukua kutoka Man United.


Baada ya kauli ya rais huyo, inaonyesha wazi ndoto za Ronaldo kurudi Man United zimeyeyuka na sasa Chelsea, PSG na Man City ndiyo zinaopewa nafasi ya kumchukua.


Kuna taarifa, Chelsea wameshaanza mazungumzo na Real Madrid na rais huyo amekuwa wa kwanza kutoa siri na mwenyewe amethibitisha huenda baada ya wiki moja kila kitu kikawa hadharani kama Ronaldo atabaki au kuondoka.

Tayari Mourinho ameshaagiza mazungumzo yafanyike kumnasa Wayne Rooney wa Man United na Cavani wa Napoli.
 


Ronaldo amewahi kulalama kwamba hana raha Madrid, lakini baada ya mazungumzo na uongozi alirejea katika hali yake na kucheza soka safi.
Hivi karibuni ilielezwa kwamba yuko katika mahusiano mabaya na Mourinho, lakini yeye akakanusha.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic