May 18, 2013



Sure Boy akithibiti mpira mbele ya kiungo wa zamani wa Simba, Emmanuel Okwi
Kocha Mkuu wa Azam FC, Stewart John Hall ameamua kumuacha nje kiungo wake nyota, Salum Abubakari ‘Sure Boy’ kabla ya mechi ya leo ya kufunga msimu dhidi ya JKT Oljoro.

Mechi hiyo inapigwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha na Sure atakuwa nje ya kikosi.


“Nimefanya hivyo kama sehemu ya kumpumzisha, amecheza mechi nyingi sana kwa msimu.

“Halafu baada tu ya mechi atalazimika kuingia kambi timu ya taifa, hivyo nimeamuacha Dar es Salaam ili aendelee na mapumziko,” alisema Hall raia wa Uingereza.

Kabla ya hapo, Hall aliamua kuwaruhusu wachezaji wake wote wa kigeni kurejea makwao na kutaka mechi yao leo ya kufunga msimu wacheze wazawa hasa wale ambao hawakuwa wakipata nafasi mara kwa mara kwa msimu wote.

Azam FC imemaliza msimu ikiwa katika nafasi ya pili kama ilivyokuwa msimu uliopita na kujihakikishia nafasi ya kucheza michuano ya kimataifa mwakani.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic