May 3, 2013



Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inakutana Mei 9 mwaka huu jijini Dar es Salaam kupokea na kupanga utekelezaji wa maagizo ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa) kuhusu uchaguzi wa shirikisho.

Kikao hicho cha dharura chini ya Uenyekiti wa Rais wa TFF, Leodegar Tenga kitakuwa na ajenda hiyo moja tu katika kuhakikisha utekelezaji wa maelekezo ya Fifa unafanyika haraka ili uchaguzi ufanyike ndani ya muda uliopangwa.


Fifa katika maelekezo yake imetaka kwanza ziundwe Kamati ya Maadili na Kamati ya Rufani ya Maadili kabla ya kuingia kwenye mchakato wa uchaguzi wa Kamati mpya ya Utendaji ya TFF.

 Fifa imeagiza uchaguzi uwe umefanyika kabla ya Oktoba 30 mwaka huu.

Tayari shirikisho hilo lililotuma wajumbe wake hivi karibuni kuja nchini kutatua mgogoro wa uchaguzi wa TFF na tayari limeagiza kurudiwa kwa mchakato huo.

TFF kukutana, maana yake watajadili ambayo walielezwa na kutakiwa kuyatimiza ili kufanya mambo yaende katika mstari.

Wagombea wote wakiwemo wale waliokuwa wameondolewa wamekubaliwa kuchukua fomu na kugombea.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic