May 16, 2013



 
Gumzo lilikuwa ni uchezaji wa Fernando Torres na fedha pauni milioni 50 walizotoa Chelsea kumhamisha kutoka Liverpool.

Ingawa ilionekana kama hana msaada, lakini tayari amefanya kazi kubwa kuisaidia timu hiyo kutwaa makombe mawili makubwa.

Ubingwa wa Ligi ya Mabingwa msimu uliopita baada ya kuifunga Bayern Munich katika fainali baada ya kuing’oa Barcelona katika nusu fainali.

Lakini mchango wake pia umeonekana katika michuano ya Europa League ambayo jana Chelsea wametawazwa kuwa mabingwa.

Katika mechi ya fainali, Torres amefunga bao la kwanza lakini amekuwa msaada mkubwa katika mechi hadi kufikia fainali.

Maana yake ameifikisha Chelsea kuweka rekodi ya mafanikio makubwa zaidi barani Ulaya kuliko klabu yoyote.

Hakuna timu ya England ambayo hata imejaribu kusogelea mafanikio hayo ya kuingia fainali za Ligi ya Mabingwa na Europa League kwa miaka miwili mfululizo na kutwaa makombe yote.

Maana yake, Chelsea hawana sababu ya kujuta kwa Torres ambaye akiwa na timu yake ya taifa ya Hispania, ameishatwaa ubingwa wa Kombe la Dunia na ule wa Ulaya.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic