May 16, 2013



 
Muda (kushoto) akiwa na Achimpate wakijiandaa kukwea pipa kwenda Ujerumani, wiki iliyopita.

Kocha Mkuu wa Taifa Stars ametangaza kikosi kitakachowavaa Morocco Juni 8 mjini Marakesh. Lakini wachezaji wawili makind ndiyo gumzo.
 
Poulsen raia wa Denmark amewaita wachezaji kadhaa akiwemo kipa wa Yanga, Ally Mustapha ‘Barthez’ na makinda wawili kutoka Azam FC na Mtibwa Sugar.

Kocha huyo amewatema kadhaa akiwemo mkongwe Shabani Nditi wa Mtibwa Sugar.


Kikosi hicho kitaanza safari kwa kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Sudan mjini Addis Ababa, Ethiopia Juni 2 kabla ya kwenda Morocco katika mechi hiyo kuwania kucheza Kombe la Dunia.

Kikosi kamili hiki hapa:

MAKIPA; Juma Kaseja, Mwadini Ally Mwadin, Aishi Manula na Ally Mustapha Barthez,

MABEKI; Erasto Nyoni, Aggrey Morris, Waziri Salum(Azam), Vicent Barnabas (Mtibwa), Nadir Haroub ‘Cannavaro, Kelvin Yondani (Yanga), Shomari Kapombe (Simba).
VIUNGO; Mrisho Ngassa, Amri Kiemba, Mwinyi Kazimoto, Haruna Chanongo (Simba), Simon Msuva, Athuman Idd ‘Chuji,’ Frank Domayo (Yanga), Khamis Mcha, Salum Abubakar ‘Sure Boy,’ Mudathir Yahaya (Azam).
WASHAMBULIAJIA; Mbwana Sammata, Thomas Ulimwengu, (TP Mazembe), John Bocco (Azam), Zahoro Pazi (Lyon) na Juma Luizio (Mtibwa Sugar).

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic