May 18, 2013



Uongozi wa Yanga, uko katika mchakato wa kuhakikisha wake, wapenzi na watoto wa wachezaji wanakuwa uwanjani leo kushangilia pamoja kombe la ubingwa wa Ligi Kuu Bara.

Yanga imeamua kutumia utaratibu huo ikiwa ni sehemu ya kufuata kama ambavyo timu nyingi za Ulaya hufanya.

“Mawasiliano yameishafanyika na sasa tuko katika hatua za mwisho kukamilisha kuhusiana na wake, watoto na wapenzi wa wachezaji kuwa pale uwanjani.


“Tumeamua kufanya hivi kama sehemu ya utaratibu kwa kuwa mambo yanabadilika duniani kote, umeona namna mambo yanavyokwenda kila sehemu.

“Hivyo ni vizuri kuiga vitu vizuri na ndiyo maendeleo yenyewe, tunaamini wengine watatuiga sisi wakati mwingine,” kilieleza chanzo kutoka ndani ya Yanga.

Kama watafanya hivyo leo, Yanga itakuwa timu ya kwanza kutumia utaratibu huo hapa Tanzania.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic