Katika hali isiyo ya kawaida, Uwanja wa Mabatini unaotumiwa na Ruvu
Shooting kama uwanja wa nyumbani, umetawaliwa na wavuta bangi.
Katika mechi ya Ruvu dhidi
ya Kagera Sugar lilishuhudia vijana kadhaa waliojitenga kwenye sehemumoja ya
jukwaa uwanjani hapo, wakivuta kilevi hicho wakati mechi ikiendelea.
Kama hiyo haitoshi, baada ya muda walianza kutoa lugha kali kuelekea kwa wachezaji
wa Kagera Sugar kila walipokuwa wakigusa mpira.
Aidha, tukio la kushangaza lililootokea uwanjani hapo ni gazeti hili
kushuhudia wachezaji wakiogea katika chumba kisicho na mlango huku wengine
wakijisitili kwa kujipanza kwenye kuta za jukwaa la mashabiki kushoto mwa
jukwaa kuu, sehemu ambayo haijengwa vema.
Suala la matatizo ya viwanja vibovu katika Ligi Kuu Tanzania Bara ni
tatizo sugu lakini wamiliki na waangalizi wa viwanja hivyo wamekuwa wagumu
kutoa ufafanuzi na kufanyia marekebisho.
0 COMMENTS:
Post a Comment