SAFU NZIMA YA UONGOZI WA TASWA IKIONGOZWA NA MWENYEKITI, JUMA PINTO (KATIKA WALIOKAA), KUSHOTO NI MAKAMU MWENYEKITI, MAULID KITENGE, KULIA NI KATIBU MKUU, AMIR MHANDO 'MGOSI'. |
Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA), kinatoa
pongezi kwa uongozi mpya wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) uliochaguliwa
Jumapili iliyopita.
Tunaungana na wapenda michezo na Watanzania kwa ujumla kuitakia
kila la heri Kamati ya Utendaji ya TFF na shirikisho hilo kwa ujumla chini ya
Rais mpya Jamal Malinzi na Makamu wake, Wallace Karia.
TASWA inaamini Malinzi, Karia na wajumbe wao ni wazoefu na ni watu
wenye kujua mambo mengi yanayohusu mpira wa miguu nchini, hivyo tunaamini
watakuwa viongozi wazuri kwa nafasi zao katika kuhakikisha shirikisho hilo
linasonga mbele.
Tunawatakia kila la heri Wajumbe wote wa Kamati ya Utendaji, huku
tukiamini hawatawaangusha Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa TFF waliowaamini kushika
nafasi hizo.
TASWA na waandishi wa habari za michezo kwa ujumla hapa nchini
tunaahidi kuwapa ushirikiano wa kutosha ili watekeleze majukumu yao ipasavyo.
0 COMMENTS:
Post a Comment