PICHA ALIYOPIGA INIESTA |
Kiungo nyota wa Barcelona na timu ya taifa ya Hispania, Iniesta
ameonyesha furaha kurejea na kuliona live goli alilofunga bao siku ya mwisho ya
michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2010.
Iniesta alipiga picha za lango hilo ambalo liko kwenye Uwanja wa Soccer
City, Johannesburg, Afrika Kusini.
“Nimefurahi kurudi hapa,” aliandika kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter.
Iniesta na
kikosi cha Hispania ambao ni mabingwa Dunia walikuwa nchini humo kucheza mechi
ya kirafiki waliyolala kwa bao 1-0 dhidi ya wenyeji Bafana Bafana.
Katika
michuano hiyo mwaka 2010, Hispania ilishinda bao 1-0 katika fainali na kubeba
kombe hilo.
0 COMMENTS:
Post a Comment