Kiungo Salum Telela wa Yanga, anatarajiwa kurejea dimbani kuendelea
kuitumikia timu yake hiyo Januari, mwakani katika mzunguko wa pili wa Ligi Kuu
Bara.
Telela aliumia enka ya mguu wa kulia kwenye mechi dhidi ya Tanzania
Prisons ambapo ilimlazimu kukaa nje ya uwanja kwa muda wa mwezi mzima ambapo
baada ya kupona anahitaji mazoezi mepesi kwa ajili ya kukaa sawa ili apone
kabisa.
Telela amesema amepona kabisa, lakini amepewa muda wa kujiweka sawa zaidi
kwa ajili ya kurudi vema msimu ujao kwa sababu muda aliopewa na mechi
zilizobaki ni chache.
“Nimepewa muda wa kupumzika kwa ajili ya kujiweka vema ili nikirudi
nianze upya, kwa hiyo sitakuwepo mpaka mzunguko huu unamalizika. Nitakuwepo kwenye mzunguko wa pili Januari,”
alisema Telela.
Zimebaki mechi mbili kwa kila timu kumaliza mechi zake za mzunguko wa
kwanza ambapo mzunguko wa pili unatarajiwa kuanza Januari 25 mwakani, kwa Yanga
kuivaa Ashanti, mechi itakayopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar.
0 COMMENTS:
Post a Comment