Mabingwa wa Ulaya, Bayern Munich
wameonyesha wamepania kuendelea kuwa mabingwa wa Ulaya baada ya ushindi safi wa
mabao 3-0 dhidi ya wapinzani wao wakubwa Borussia Dortmund.
Bila ya kujali Dortmund wanaovaa njano
na nyeusi wako nyumbani, Bayern wamewatungua bao hizo huku wakiwaonyesha soka
safi.
Mabao ya Bayern yalifungwa na Mario
Gotze katika dakika ya 66, kumbuka nyota huyu amejiunga na Bayern akitokea
Dortmund, msimu huu.
Baadaye Arjen Robben akaongeza msumari
wa pili katika dakika ya 85, huku ikionekana Dortmund ikutafuta bao la kufutia
machozi, Bayern ikaongeza la tatu katika dakika ya 87, Thomas Muller akiingia
kimiani.
Pamoja na kuwa ugenini, Bayern
walitawala mchezo huo kwa muda wote wakianzia kipindi cha kwanza na wenyeji
walikuwa wakifanya mashambulizi machache ambayo yalionyesha kuwa na nguvu
lakini hayakuzaa matunda.
0 COMMENTS:
Post a Comment