Mwenyekiti aliyesimamishwa Simba, Ismail
Aden Rage amekaidi agizo lililotolewa na TFF la kuitisha mkutano wa dharura wa
wanachama ndani ya siku 14.
Pamoja na hivyo, Rage amesema kama TFF
itaendelea kumshinikiza, basi mara moja atajiuzulu.
Rais wa TFF, Jamal Malinzi alimsisitiza
Rage kufanya hivyo ili kulitatua tatizo lililojitokeza. Rage ameyasema hayo katika mkutano na waandishi wa habari uliomalizika punde katika makao makuu ya Simba jijini Dar.
Pia Malinzi akaahidi kutuma mjumbe wa
TFF ambaye atakwenda kusimamia mkutano huo huku akisisitiza suala la haki
lichukue nafasi.
Kaka Suma kweli kiboko hadi TFF Dah!!!
ReplyDelete