Beki wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ amesema sababu kubwa ya kutemwa
kwake kwenye kikosi cha Zanzibar Heroes siyo suala la kushuka kiwango ila ni
kwa kuwa hakurudisha fedha walizogawana wachezaji wa timu hiyo mara baada ya
kushika nafasi ya tatu katika Kombe la Chalenji, mwaka jana.
Cannavaro ni mmoja wa wachezaji waliotemwa katika kikosi hicho
kinachojiandaa kwa ajili ya michuano hiyo tena ambayo inatrajiwa kuanza Novemba
27, mwaka huu nchini Kenya.
“Kocha (Salum) Bausi ameacha kuniita siyo kwa sababu ya kiwango ila ni
kile kisa cha kutorudisha fedha tulizojigawia za mshindi wa tatu katika
michuano iliyopita,” alisema Cannacaro.
Wachezaji wa Zanzibar Heroes waligawana fedha hizo kwa kile walichodai
zingefika kwa viongozi wala wasingezipata.
“Mbona timu ya taifa nipo na Yanga napata namba kama kawaida na mimi ndiyo
nahodha. Mimi nimeridhika kutoitwa, kwa sababu timu ina wachezaji wengi wazuri.
Naitakia kila la kheri timu yangu na wala sina kinyongo nayo,” alisema.
SOURCE: CHAMOPIONI
0 COMMENTS:
Post a Comment