Kocha Mkuu wa Azam FC, Stewart Hall amefunguka kuwa atamuweka nje mshambuliaji
wake mkongwe, Gaudence Mwaikimba kwenye kikosi chake kwa kuwa mchezaji huyo
amechoka baada ya kumtumia kwenye mechi nyingi.
Inaelezwa kuwa Mwaikimba ameanza mapumziko hayo kwenye mechi ya Ligi Kuu
Tanzania Bara ya timu yake dhidi ya Simba, Jumatatu ya wiki hii.
Stewart alisema kuna uwezekano wa Mwaikimba kuwa nje katika mechi mbili
zijazo za kukamilisha mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Ruvu
Shooting na Mbeya City.
“Mwaikimba hana majeraha yoyote, nimeamua kumpumzisha katika mechi hizi
tatu, kuanzia ile ya Simba na hizi mbili zilizobaki za kumalizia mzunguko wa
kwanza wa ligi, sababu ni kuwa ametumika kwenye mechi nyingi,” alisema Stewart.
0 COMMENTS:
Post a Comment