Imeelezwa kuwa dau la usajili la kipa
namba moja wa Mtibwa Sugar, Hussein Sharifu ‘Casillas’, ndilo limesababisha
ashindwe kutua kuichezea Simba inayomwania.
Kipa huyo ameingia kwenye orodha ya
makipa wanaowaniwa vikali na timu hiyo, akiwemo Ivo Mapunda anayeichezea Gor
Mahia ya Kenya.
Akizungumza na Championi Jumatano, Casillas
alisema kuwa yeye hana tatizo kwani Simba walishamfuata na tayari ameshawatajia
dau lake, kilichobaki wao wenyewe wakamilishe kiasi hicho cha fedha yeye avae
jezi nyekundu.
Casillas alisema yeye hana haraka,
anawasubiri mara watakapokubaliana katika kutoa dau hilo ambalo ni siri,
akaongeza kwamba mara moja atasaini mkataba wa kuichezea timu hiyo katika
dirisha dogo.
“Meneja wangu tayari amewatajia Simba
dau la usajili tunalolitaka, hivyo tunawasubiri watakapokuwa tayari watoe
haraka fedha hiyo nami nitasaini mkataba husika.
“Mimi ninachoangalia ni maslahi pekee,
siyo kingine na sina haraka, wenyewe wamalizane na meneja wangu tu, kama
wakishindwa nitaendelea kuichezea timu yangu ya Mtibwa Sugar,” alisema Casillas
ambaye aliitwa kwenye kikosi cha kwanza cha timu ya taifa kabla hajatemwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment