Timu ya Mtibwa Sugar imebariki aliyekuwa
kiungo wao, Awadhi Juma, kutua katika kikosi cha Simba.
Awadhi ambaye aliichezea Mtibwa Sugar
kabla ya kutua Thailand katika klabu ya Criracha FC, inayoshiriki Ligi Daraja
la Kwanza, ametua Simba kwa mkataba wa miaka miwili.
Mratibu wa Mtibwa Sugar, Jamal Bayser, alisema hawana shida na mchezaji huyo
kutua Simba kwani atawasaidia katika mzunguko wa pili, pia kwa upande wao
walishamalizana naye na ni mchezaji huru.
“Awadhi ni mchezaji mzuri na hakuna
shida kutua Simba kwa kuwa ni mchezaji huru, alishamaliza mkataba na sisi,
hivyo atawasaidia sana Simba kwani ni mchezaji mzuri.
“Sisi kama Mtibwa tunatarajia kukutana
ndani ya wiki hii kujadili ripoti ya kocha Mecky Maxime kwa ajili ya kuanza
mchakato wa usajili wa wachezaji wapya,” alisema Jamal.
0 COMMENTS:
Post a Comment