Beki wa zamani wa Arsenal, William Gallas amefanya
mazoezi pamoja na beki Mtanzania Shomari Kapombe.
Kapombe na Gallas wamefanya mazoezi kwenye kikosi
cha daraja la nne nchini Ufaransa cha AS Cannes anachokichezea Mtanzania huyo.
Katika mazoezi hayo, Kapombe alikuwa kikosi kimoja
na Gallas ambaye aliwahi kung’ara Ligi Kuu England pia akiwa na Spurs.
Mtanzania huyo aliyekuwa ameumia, tayari amerejea
kazini na alianza katika mechi ambayo timu yake ilitoka sare ya bao 1-1 wiki
iliyopita.
0 COMMENTS:
Post a Comment