TAMBWE |
Kuwepo kwa taarifa kwamba wako sokoni na
Yanga imekuwa ikinyata, kumeifanya Simba kufunguka.
Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage
amesema wachezaji hao hawauzwi.
“Hawauzwi na kama kuna mtu anafikiri
hivyo basi anajisumbua,” alisema.
“Kweli Simba tuna sera ya kuuza
wachezaji lakini kwa hawa hatuhitaji na badala yake tunaboresha kikosi ili
tupambane kwenye ligi.”
Tambwe ndiye tegemeo katika ufungaji
Simba, anaongoza wapachika mabao wa Ligi Kuu Bara, lakini Chanongo ni kati ya
wachezaji wanaochipukia kwa kasi katika soka nchini na amekuwa msaada mkubwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment