IVO (ALIYEANGUKA) AKIWA MAZOEZINI NA GOR MAHIA KWENYE UWANJA WA CITY JIJINI NAIROBI, JUMAMOSI ILIYOPITA |
Kipa wa Gor Mahia, Ivo Mapunda leo
ameichezea tena Taifa Stars baada ya kuachwa kwa zaidi ya miaka mitatu.
Katika mechi mazoezi dhidi ya Future
Taifa Stars, Ivo aliingia kipindi cha pili kuchukua nafasi ya Ally Mustapha ‘Barthez’
aliyekuwa tayari kafungwa bao 1-0 la Elias Maguri.
Ivo alifanikiwa kudaka kwa dakika zote
45 bila ya nyavu zake kutikiswa.
Awali, Poulsen aliamua kumtema Ivo
lakini baadaye iligundulika TFF haikuwa imefikisha barua katika Shirikisho la
Soka la Kenya (FKF) ambalo lingepeleka kwa timu yake.
Ivo aliamua kuzungumza na TFF ambao
walimueleza kuhusiana na kuachwa kwake, lakini baadaye inaelezwa alizungumza na
Poulsen ambaye baadaye aligundua kipa huyo hakuwa na tatizo na kumrudisha.
0 COMMENTS:
Post a Comment