Nyota wa Yanga, Jerry Tegete na Said
Bahanuzi, wanatarajiwa kukiongoza kikosi cha vijana cha timu hiyo ‘U-20’,
kitakachoshuka dimbani kesho kuchuana na Saigon, katika mchezo wa fainali Kombe
la Etihad ‘Street Soccer Cup’.
Katika mchezo huo, utakaopigwa kwenye Uwanja
wa Mwananyamala, Yanga walitinga hatua hiyo baada ya kuwabamiza Faru FC kwa
mabao 6-2 huku Saigon wakifuzu kwa kuwachapa Makumbusho Talents kwa mabao 4-3.
Wakati Tegete na Bahanuzi wakiongoza
safu ya Yanga, Saigon wanajivunia uwepo wa straika wa Mtibwa Sugar, Mohamed
Mkopi, ambaye alifunga mabao yote ya Siagon dhidi ya Talents.
Akithibitisha uwepo wa nyota hao,
mratibu wa michuano hiyo Saleh Dunga alisema: “Tayari wamethibitisha hilo,
wamekuja baada ya kuona wachezaji wengi wapo kwenye Michuano ya Uhai,
inayoendelea jijini Dar,” alisema Dunga na kuongeza kuwa pia kutakuwa na nyota
wengine wa ligi kuu.
Bingwa ataondoka na kiasi cha Sh
milioni 2 na kombe, wa pili atapata Sh milioni moja na watatu akiweka kibindoni
laki tano.
0 COMMENTS:
Post a Comment