Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Kim Poulsen
amesema kipigo cha bao 1-0 walichokipata kikosi hicho ni changamoto.
Stars imelala kwa bao 1-0 dhidi ya
Future Taifa Stars katika mchezo wa kirafiki uliochezwa leo kwenye Karume
jijini Dar.
Akizungumza jioni hii, Poulsen alisema
ushindani wa timu hizo mbili ulionyesha kuna kitu na waliofungwa wanapaswa
kujiuliza.
“Ilikuwa mechi nzuri na utaona namna
upinzani ulivyokuwa, lakini ni sehemu ya changamoto kwa walio katika kikosi cha
Taifa Stars,” alisema.
“Tuna mechi ngumu dhidi ya Kenya, hivyo
lazima tuwe tayari kabla ya kucheza nao kwa kuwa tutakuwa nyumbani,” alisema.
Taifa Stars itawavaa Harambee Stars
Jumanne ijayo kwenye Uwanja wa Taifa katika mechi ya kirafiki inayosubiriwa kwa
hamu na mashabiki.
0 COMMENTS:
Post a Comment