OKWI MAZOEZINI NA YANGA LEO ASUBUHI |
Baada ya
hadithi nyingi za Mwenyekiti wa Simba aliyesimamishwa, Ismail Aden Rage, Okwi
ameweka tayari rekodi mbili na Yanga.
Moja ilikuwa
jana alipovaa kwa mara ya kwanza jezi ya Yanga na kupokelewa na viongozi wa
timu hiyo.
Lakini leo,
ameweka nyingine baada ya kufanya mazoezi na timu hiyo akiwa chini ya Kocha
Mholanzi, Ernie Brandts.
Katika mazoezi
hayo kwenye Uwanja wa Bora Kijitonyama jijini Dar, Okwi alikuwa kivutioo
kikubwa na watu wengi walijitokeza kumshuhudia.
Rage amekuwa
akisisitiza Okwi hatocheza Yanga, huenda kesho kauli yake hiyo ikafutika kabisa
atakapoichezea Yanga katika mechi ya Nani Mtani Jembe dhidi ya Simba.
Baada ya
mechi hiyo, kitakachosubiriwa ni Okwi kucheza mechi ya mashindano, suala ambalo
Rage atakuwa amepoteza cha kusema.
Rage
ameendelea kusisitiza kwamba Okwi hatakiwi kucheza Simba, lakini Yanga
wanaendelea na mambo yao kama kawaida.
0 COMMENTS:
Post a Comment