Mshambuliaji wa Yanga, Emmanuel Okwi,
raia wa Uganda ametimka nchini na kurudi kwao Uganda kufuatia matatizo ya
kifamilia yanayomkabili.
Okwi alitua Yanga wiki iliyopita ambapo
alicheza mechi ya ‘Nani Mtaani Jembe’ dhidi ya Simba, mchezo ambao timu yake
ilichapwa mabao 3-1.
Kocha
Msaidizi wa Yanga, Fred Minziro, alisema Okwi aliondoka mara baada ya mchezo wa
kirafiki dhidi ya Simba na kudai kuwa atarudi mara baada ya Krismasi.
“Okwi ameondoka nchini amerudi kwao
kufuatia matatizo ya kifamilia na atarudi baada ya Krismasi.
“Ameomba ruhusa kwa uongozi na umempa ruhusa
hivyo na tunaamini kuwa atakuwa kwenye mazoezi ya timu hii Ijumaa ijayo,”
alisema Minziro.
0 COMMENTS:
Post a Comment