Siku chache baada ya kutimuliwa kazi, aliyekuwa Kocha wa Rhino Rangers
Sebastian Nkoma, ameibuka katika fani ya ualimu wa shule ambapo sasa
anafundisha masomo ya ziada ‘twisheni’ katika shule za sekondari.
Nkoma alisema ualimu ni moja taaluma
alizonazo, hivyo kujiweka kando na soka ndiyo njia ya kuendeleza taaluma
nyingine, ambapo kwa sasa ni mwalimu katika shule za sekondari za Aga Khan na
Benjamini Mkapa za Dar es Salaam.
“Maisha siyo soka tu, mimi ni mwalimu pia. Hii ndiyo taaluma yangu na
kwa sasa ndiyo kazi ninayoifanya. Ninafundisha shule mbalimbali kuna Aga Khan,
Benjamini Mkapa pote nina vipindi,” alisema kocha huyo.
SOURCE: CHAMPIONI
0 COMMENTS:
Post a Comment