Klabu ya Simba ipo kwenye mikakati ya kutafuta nyumba kwa ajili ya
kocha wao, Mcroatia Zdravko Logarusic na wachezaji wapya wa timu hiyo.
Ofisa Habari wa Simba, Stanley Philip
amesema uongozi kwa sasa unalifuatilia suala hilo kwa kutafuta nyumba ya kisasa
kwa ajili ya kocha na wachezaji wapya wa kikosi hicho.
Alisema mchakato huo ulianza mapema lakini hawakupata iliyokidhi
viwango hivyo watahakikisha watakaporejea kwenye Michuano ya Mapinduzi atafikia
nyumbani kwake.
Upande wa beki wao Mkenya, Donald Musoti, Philip alisema amerejea kwao kuchukua vitu vyake alivyoviacha
kisha atarejea leo Ijumaa.
“Tupo kwenye mchakato wa
kutafuta nyumba ya kisasa ya Kocha Loga pamoja na wachezaji wengine wapya
waliojiunga nasi haijalishi maeneo gani ilimradi tu nyumba iwe na ubora,”
alisema Philip.
0 COMMENTS:
Post a Comment