Ingawa amepata nafuu lakini hali ya
Edibil Lunyamila bado si nzuri sana.
Leo asubuhi daktari alitoa mirija ya
mashine za kupumulia na baadaye akazirudisha tena baada ya kuona analazimika kufanya
hivyo.
Baadhi ya watu wameendelea kujitokeza
kumjulia hali mchambuzi huyo wa soka wa gazeti
la Championi katika hospitali ya Mwananyamala jijini Dar.
Lunyamila, nyota wa zamani wa Yanga&Simba,Mtibwa
Sugar na Taifa Stars bado hali yake si nzuri na matibabu yake pia yanahitaji
fedha.
Hivyo watu wanaoweza kumsaidia
wametakiwa kujitokeza na kufanya hivyo ili awe na uhakika wa matibabu.
mungu amjaalie aweze kupona haraka inshaallah
ReplyDelete