March 29, 2014


Mshambuliaji nyota wa Real Madrid ametengeneza bonge la tangazo akiwa na gwiji la soka duniani Pele.

Tangazo hilo limefanywa ndani ya moja ya ndege kubwa zaidi duniani inayomilikiwa na Shirika la Ndege la Emirate maarufu kama Fly Emirates.

Tangazo hilo linamuonyesha Ronaldo akiwa katika moja ya baa za ndege hiyo baada ya kuoga na kuvaa kitanashati tokea ndani ya chumba chake.
Akiwa pale baa, baadaye anaungana na Pele lakini anatokea mtu na kumuomba Pele ampige picha kna Ronaldo huku akionyesha kuwa amemsahau Pele.


Emirates ambao ni wadhamini wakuu wa Real Madrid wanajiandaa vilivyo kuhusiana na Kombe la Dunia litakalofanyika kuanzia mwezi wa sita nchini Brazil.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic