Kipa wa Chelsea, Petr Cech hataitumikia timu hiyo katika mechi
yoyote msimu huu.
Cech amewekwa nje msimu wote hadi mwisho kutokana na majeraha
aliyoyapata katika mechi ya kwanza ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya
dhidi ya Atletico Madrid.
Taarifa zimeeleza, kutokana na maumivu hayo baada ya kupatiwa
matibabu kwenye hospitali moja mjini Madrid, kipa huyo atalazimika kuikosa
Chelsea hadi mwisho wa msimu.
Lakini bahati mbaya tena kwa Chelsea, itamkosa nahodha wake John
Terry ambaye aliumia katika mechi hiyo.
Imetangazwa, Terry hatacheza mechi ijayo dhidi ya Atletico Madrid
jijini London.
Hivyo Chelsea, itakuwa na nafasi ya kumtumia tena, iwapo tu
itavuka na kuingia fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kuwa anatarajiwa kuwa
fiti.
0 COMMENTS:
Post a Comment