April 6, 2014

BANGO HILI LILIWEKWA MKWAKWANI, LEO WAKATI COASTAL UNION IKIIVAA MGAMBO. 

BAADHI YA MASHABIKI WA COASTAL UNION WAMEAMUA KUCHUKUA UAMUZI WA KUANDIKA BARUA KUUSHITAKI UONGOZI WA KLABU YAO KWA SHIRIKISHO LA SOKA TANZANIA (TFF).

UAMUZI WA MASHABIKI HAO, WAKIONGOZWA NA KATIBU WAO ABDULLATIF OMAR FAMAU UMETOKANA NA UAMUZI WA KATIBU MKUU WA COASTAL UNION, KASSIM EL SIAGI KUWAZUNGUSHA KUHUSU KUPATA UANACHAMA.

FAMAU AMESEMA WAMEKUWA WAKIFANYA KAZI YA ZIADA KUPATA UANACHAMA LAKINI EL SIAGI AMEKUWA AKIWAZUNGUSHA.
KATIKA BARUA HIYO AMBAYO SALEHJEMBE IMEINASA, INAELEZA KILA KITU KUHUSIANA NA MALALAMIKO HAYO YA MASHABIKI HAO WANAOPIGWA CHENGA KUPEWA UANACHAMA BILA YA SABABU ZA MSINGI. ISOME..

BARUA YA WAZI KWA KATIBU MKUU WA COASTAL UNION FOOTBALL CLUB
                                                                                                                                                                                         WAPENZI WA COASTAL FC
                                                                                                                                                                                   P.O.BOX 5152. TANGA.
                                                                                                                                 
COASTAL UNION FC
P.O.BOX 2066, TANGA.
07.04.2014.

KATIBU MKUU
YAH: MAOMBI YA KADI ZA UANACHAMA KATIKA CLUB YA MPIRA WA MIGUU  YA COASTAL UNION.
Kichwa cha habari hapo juu kinahusika. Sisi baadhi ya wapenzi wa coastal union FC ya Tanga. Tumeamua kuandika barua hii kwa katibu mkuu wa coastal union F  na itakuwa ni barua ya wazi ambayo itaonekana kwenye magazeti na kuzungumzwa katika vyombo vya habari ili kilio chetu kisikike na wadau wote wa michezo. Pia barua hii tutaipeleka TFF mkoa wa Tanga na Afisa tamaduni na michezo wa wilaya ya Tanga. Tumeandika barua hii kwa sababu zifuatazo.

Ukweli ni kwamba hatukuwa na umoja ambao umepanga kuomba kadi kwa pamoja bali halii hii ya kuungana kwa wapenzi wenye atizo la kutokuwa na kadi imekuja baada ya wapenzi wa coastal takribani kumi kukutana hapo club wote wakiwa na nia ya kutaka kupata kadi za uanachama wa coastal. 

Lakini kwa bahati mbaya kila tulipofika hapo club hatukufanikiwa kumpata mtu yeyote anayehusika na club akiwa katiaka ofisi za club, bali tulipewa mwongozo na fundi nguo aliyepo hapo nje ya club. Kuwa mkimtaka katibu basi mpigieni simu au kama kuna maagizo yeyote basi niachieni mimi nitamfikishia. Sisi hatukuridhika kumwachia maagizo yetu fundi nguo bali tuliamua kumpigia simu marakwamara. Lakin kwa bahati mbaya simu ya katibu mara nyingi inakuwa haipatikani. Na ikipatika basi haipokelewi.

Baada ya siku mbili tatu za kujaribu kumpigia simu katibu, mimi mwandishi wa barua hii (Abdullatif Famau) nilipokea simu kutoka kwa katibu wa coastal union FC. Na maongezi yalikuwa hivi:
Katibu: hello… nimeona missed call zako nani mwenzangu?
Abdullatif: mimi naitwa Abdullatif Famau; nilikupigia simu mara kadhaa baada ya kufika ofisini kwako takribani week mbili sasa lakini sijakupata, sasa lengo la kukupigia simu niI kutaka kupata card za uanachama wa timu yetu ya Coastal FC. Na bahati nzuri kuna watu zaidi ya kumi pia wanataka hizo kadi.
Katibu: sawa Abdul nimekuelewa, lakini hivi sasa tumesitisha mpango wa kutoa kadi kiholele, kwani tumesikia kuna watu wamepanga kuja katika timu yetu na kutuletea vurugu. Club ilikuwa mbovu ina vumbi, haina maji na taa sisi tumetengeneza club tukarudisha maji na Taa, timu ilikuwa katika low division sisi tukaipandisha mpaka ligu kuu, sasa hatutakubali waje watu ambao hatuwajui na kutuharibia timu yetu.
AbdulLatif: ooh ok, sasa mwalimu (katibu ni mwalimu wa shule) watu wenyewe wanaotaka card wote unatufahamu tulichelewa tu kufuatilia hizo card… labda ni utaratibu gani mbao mmeuandaa ili tuweze kupata kadi?
Katibu: utaratibu tuliopanga  ni kila mtu anayetaka kuwa mwanachama wa coastal union lazima ajaze fomu maalum na kisha atajadiliwa katika mkutano mkuu wa wanachama kama awe mwanachama au la..!
Abdullatif: ooh, ok mwalimu. Sasa ni lini hizo form zitakuwa tayari ili niwaambie jamaa siku ya kuja hapo club?
Katibu: namba yako ninayo,  form zikiwa tayari nitakufahamisha. Sawa Abdul..?
Abdullatif: sawa katibu… ahsante sana.. kwaheri…!

Maongezi yakaishia hivyo. Na mimi niliwataarifu jamaa wote ambao tulikutana club kwa nia ya kutaka card.
Tukasubiri zaidi  ya week kupigiwa simu ili kujulishwa utayari wa  fomu. Na pia kila tulipokua tukipata muda tunapita club ili kumjulia katibu kuhusu fomu lakini kwa bahati mbaya hatukuwahi kumuona katibu akiwa club.
Sasa tuliamua kuunda umoja wa wapenzi ambao hatuna kadi na kuhakikisha tunapata kadi kwa haraka iwezekanavyo. Ili tuweze kushiriki mkutano mkuu wa wanachama ambao utakuwa ni hivi karibuni. Tuliamua tuitane sote ili tuweze kujadili tufanye nini ili tupate uanachama wa coastal. Kikao chetu cha mwanzo kilikuwa katika hotel ya splendid viewl. Mnamo tarehe 22 march mwaka huu saa moja jioni mpaka saa tatu usiku. Agenda kuu ilikuwa nini tutafanya ili kupata uanachama wa Coastal union fc. Kikao hicho kilihudhuriwa na watu si chini ya 25, kila mtu alitoa mawazo yake.. laikini mawazo yaliyopita ilikuwa tumtafute tena katibu ofisini kwake na kumpigia simu na sasa atupe siku maalum ambayo fomu zitakuwa tayari.
Kweli tulifanya hivyo watu waiimpigia simu siku ya pili yake na alitoa ahadi kuwa siku ya jumanne ya week ijayo fomu zitakuwa tayari.yaani tarehe 01.04.2014.  Watu wakapeana habari kwa njia ya simu juu ya ahadi ya katibu, na tulisisitiziana kufika club sote ambao hatuna card siku hiyo ya jumanne ili kujaza fomu za maombi ya uanachama.
Ilipofika siku ya jumanne. Sio sote tuliofika club lakini zaidi ya watu kumi walifka club kwa nyakati tofauti na kwa bahati mbaya hatukufanikiwa kumpata katibu.  Kati ya sisi tulichaguana watu watano ambao wliingiaa kwenye gari yangu ili kwenda nyumbani kwa katibu baada ya kumpigia simu na ilikuwa haipokelewi na mwisho ilikuwa haipatikani kabisa. Tuliendesha gari mpaka nyumbani kwake na kwa bahati mbaya pia hatukumpata lakini tuliacha maagizo kwa mkewe kuwa wapenzi wa coastal wamefika hapa na wamekuja kwa lengo la kutaka fomu za maombi ya uanachama. Hivyo ili afahamu ni akina nani wamekwenda nyumbani kwake. Mimi nikaacha jina langu ili apewe ujumbe.
Baada ya masaa matatu nilipokea ujumbe kwenye simu yangu kutoka kwa katibu. Na mimi nilimjibu. Mtiririko wa message zetu ulikuwa hivi:
Katibu: nimepata salamu kuwa mmekuja nyumbani kundi kubwa na familia yangu imetishiwa na ujio wenu. NINAKUKATAZA KULETA GENGE NYUMBANI, HIYO IWE MWANZO NA MWISHO, AU MTANIONA MMBAYA.kama ni mambo ya coastal ni club.
Abdullatif: Pole sana mwalimu kwa kukusumbua, tusamehe kwa kufanya hivyo, ila tumekuwa tukija club kila siku kukuona lakini hatufanikiwi. Tumesikia kuna watu wamekuja nyumbani kwako na wakapata waliyoyataka, nasi tukaja huko.
Katibu: wale kadi zao zilikuwa tayari na wengine majina yao yalikuwepo tangu mwaka jana kwa ajili ya uchaguzi, Nassor aliwaombea…. Ndio niliowashughulikia….nyie wapya nitakupigia  mara tu form zikiwa tayari….
Abdullatif: ok! Ahsante mwalimu. Tutazidi kusubiri natumai hazitachelewa.

Mwisho wa majibizano ya ujumbe.

Mpaka leo tunaandika barua hii mheshimiwa Siagi (katibu) hajatufahamisha kama form ziko tayari. Hivyo basi tuanpenda kujulishwa kwa njia ya maandishi ni lini form zitakuw tayari.ili na sisi ikifikia kipindi cha mkutano mkuu tuweze kushiriki na pia kupiga kura ikitokea uchaguzi wa viongozi.
Pia tunapenda kukukumbusha bwana katibu. Utaratibu unaotuekea sisi wa kujaza fomu na kisha tujadiliwe ndio tuwe wanachama, ndio utaratibu haswaa ambao katiba ya coastal union inautambua. Rejea katiba ya C.U.F.C TOLEO LA 2010/2011. KIPENGELE CHA WANACHAMA. IBARA YA 6 na 7 (sifa na utaratibu wankupata hadhi ya uanachama)
Kitu ambacho kinatushangaza, je wanachama wote waliopo katika orodha yako wamejaza fomu na kujadiliwa na kupitishwa kuwa wanacha na mkutano mkuu? Sisi tuna ushahidi ambao unaonyesha wanachama karibia wote hawakujaza fomu na kama wamejaza basi hawakujadiliwa. Hivyo basi tuna mashaka  ya uhalali wao wa uanachama. Na tunathubutu kusema kutokana na katiba wanachama wengi sio halali bali ni bandia. Na ikiwa wanachama hao  bandia ndio waliotumika kupiga kura za kuchagua uongozi wa juu ya timu, pia tunahoji uhalali wa viongozi hao kuwa madarakani.
Kama tulivyotangulia kusema, barua hii itasomeka katika vyombo vya habari na pia TFF mkoa na AFISA TAMADUNI WA WILAYA. Hivyo tunaomba kila chombo husika iangalie haki yetu ya sisi kucheleweshwa kupatiwa fomu za maombi ya uanachama. Na ikionekana uongozi umefanya makosa, basi wawajibishwe ili iwe mfano kwa timu nyimgine za mpira ambazo zinamilikiwa na wanachama.
Ni matumaini yetu sheria itachukuas mkondo wake kunyamazisha kilio chetu.


Wako katika michezo

………………………………………………….
Mwakilishi wa wapenzi wa COASTAL UNION FC
ABDULLATIF OMAR FAMAU.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic