April 6, 2014


Mshambuliaji mwenye kasi wa Yanga, Mrisho Ngassa amepiga bao tatu au hat trick wakati Yanga ikishinda kwa mabao 5-1 dhidi ya Ruvu Shooting katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.

Ngassa amepiga bao hizo na alionekana kuwa na kasi zaidi huku akiwapa wakati mgumu mabeki wa JKT ambayo inapigania roho yake kuepuka kuteremka daraja.

Hussein Javu na Didier Kavumbagu nao walipiga mabao mengine mawili yaliyoiongezea Yanga akiba hiyo nzuri ya mabao hadi kufikisha matano.

Bao pekee linalonolewa na Fred Felix Minziro lilifungwa na Nashon Naftali.

Baada ya mechi hiyo, Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van Der Pluijm alisema amefurahishwa na ushindi huo ambao walistahili kuupata katika mechi zilizopita.


Yanga imepata ushindi huo bila ya kuwa na mshambuliaji wake, Emmanuel Okwi pamoja na kipa, Juma Kaseja ambao hawakuwepo hata kwenye benchi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic