June 3, 2014



Michael Wambura amelifikisha suala lake na mwanasheria mkongwe nchini Dokta Damas Daniel Ndumbaro kwenye Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).


Wambura amelifikisha suala hilo kwenye kamati ya maadili ya TFF baada ya Ndumbaro kufunguka Jumapili iliyopita.
Ndumbaro ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya uchaghuzi ya Simba alieleza mambo kadhaa akijibu mapigo ya Wambura ambaye awali alitangaza kumchangishia fedha ili aende akasome.

Lakini Ndumbaro akasema ameishamaliza madarasa yote na kumtaka Wambura achangishe fedha kwa ajili ya kujilipia ada kwa kuwa inamshinda.

Pia Ndumbaro akasema yeye ni mwalimu wa Wambura katika Chuo Kikuu Huria (Out) na anaujua udhaifu wake ingawa maadili yanamzuia kuutangaza hadharani.
Wambura amesema Ndumbaro alimshambulia nje ya masuala ya uchaguzi, hivyo anataka kamati hiyo ya maadili ya TFF ichukua hatua.

Sakata hilo lilianza baada ya kamati ya uchaguzi ya Simba chini ya Ndumbaro kumuengua Wambura na kutangaza kuwa alisimamishwa uanachama.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic