Wakati Kocha
mpya wa Simba, Patrick Phiri raia wa Zambia ametua nchini, angalia aliyekuwa
kocha wa timu hiyo, Zdravko Logarusic alivyoliaga jiji la Dar.
Kupitia mtandao
wa Facebook, Loga ametupia picha mbili huku akiandika “by by Tanzania),
akimaanisha bye bye Tanzania.
Loga ameiaga
Tanzania kwa picha hizo, moja akiwa ndani Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa
Julius Nyerere (JNIA) akiwa amepiga shati lake la pink na mkononi ameshikilia
kinywaji aina ya Redbull.
Picha ya pili,
Loga anaonekana kiwa amekaa kwenye beki, hapo ni kabla ya kuingia ndani ya
uwanja huo.
Kocha huyo
ameondoka na dege la Shirika la Ndege la Tukish.
Kama safari
yake imekwenda vizuri, tayari Loga atakuwa amewasili kwao salama.
0 COMMENTS:
Post a Comment