Straika wa Azam FC raia wa Burundi, Didier
Kavumbagu amesema hatawasahau walinzi wa kati wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’
na Kelvin Yondani kwa kuwa walimchezea kibabe katika mechi yao ya Ngao ya
Jamii, kiasi cha kutaka kumvunja.
Akielezea mechi hiyo iliyopita kwenye Uwanja wa
Taifa jijini Dar, Jumapili iliyopita, alisema hakufurukuta kwa kuwa wawili hao
walimchezea vibaya muda mwingi wa mchezo. Azam FC ililala kwa mabao 3-0.
“Walikuwa wakinichezea kibabe na kunikaba muda
wote kama walivyokuwa wakifanya kwa Kipre Tchetche, lakini sawa, yote yamepita.
“Mungu akipenda tutaonana tena katika ligi kuu,
na hapo ndipo nami watakapoona kazi yangu,” alisema Kavumbagu.
Raia huyo wa Burundi ametua Azam FC akitokea
Yanga ambayo alijiunga nayo akitokea Atletico ya kwao Burundi.
0 COMMENTS:
Post a Comment