Kipa wa Gor Mahia ya Kenya, Fredrick Onyango,
amesema kumkaba mshambuliaji wa Simba, Paul Kiongera si kazi lahisi.
Lakini akasisitiza, kama timu inataka kupumua,
basi ni kutompa nafasi ya kufanya mambo yake.
Kiongera anatajwa kuwa mmoja wa washambuliaji
hatari wanaotarajiwa kutamba katika Ligi Kuu Bara inayotarajiwa kuanza kesho
Jumamosi.
Kipa huyo Mkenya amesema, Kiongera ni hatari
akiachiwa nafasi. “Wanatakiwa kutompa nafasi ya kucheza na kufanya anavyotaka,
wakifanya hivyo tu watakuwa wamemmaliza.
Onyango ambaye alifungwa mabao mawili na
Kiongera wakati Simba ilipoitwanga Gor Mahia kwa mabao 3-0 katika mechi ya
kirafiki, amesema Kiongera ana mambo mengi.
“Uwezo wake ni mkubwa, ana kasi, nguvu na
anapiga mashuti. Unaweza kusema ana kiula kitu, hivyo kuwa naye makini ni jambo
zuri.”
0 COMMENTS:
Post a Comment