Simba iko katika hatua za mwisho kupata kibali cha kufanyia kazi
nchini cha kiungo wake Emmanuel Okwi raia wa Uganda.
Iwapo Simba itashindwa kupata kibali hicho leo, maana yake Okwi
hatacheza mechi dhidi ya Coastal Union kesho.
Simba inawavaa Wagosi wa Kaya kesho kwenye Uwanja wa Taifa kwenye
mechi yake ya ufunguzi wa Ligi Kuu Bara.
Rais wa kwanza wa Simba, Evans Aveva amethibitisha hilo na kueleza
linafanyiwa kazi kwa juhudi kubwa.
Okwi amejiunga na Simba akitokea Yanga ambayo ilimpata kutoka SC
Villa ya Uganda.
0 COMMENTS:
Post a Comment