Kocha Mkuu wa Yanga, Marcio Maximo amemtaka mshambuliaji wake,
Jaja kutuliza presha atakayopambana nayo mjini Morogoro.
Maximo ameamuambia Jaja awe makini na aliyeelekeza nguvu zote
kwenye mechi dhidi ya Mtibwa Sugar, leo.
“Unajua ni siku ya kwanza Jaja anaanza kucheza mikoani, kocha
ameliona hilo na ameishazungumza naye.
“Amemtaka kufuata alichofundishwa pia kuongeza ujuzi wake, tatizo
kila mtu atataka kumuona anafunga.
“Hivyo inaweza kuwa presha kubwa kwake, kocha ameliona jambo hilo,”
kilieleza chanzo tokea ndani ya Yanga.
Tayari Yanga wako mjini Morogoro kwa ajili ya mechi hiyo
inayosubiriwa kwa hamu.
0 COMMENTS:
Post a Comment