September 23, 2014


Mkosi! Simba itacheza mechi yake ya Oktoba 12 bila ya mshambuliaji wake Paul Kiongera.

Vipimo vilivyotolewa leo kwenye hospitali ya rufaa ya Muhimbili vimeeleza Kiongera ameumia sana goti lake na tayari imepitishwa apumzike wiki sita.
Hali hiyo imejulikana baada ya daktari wa Simba kusafiri na Kiongera hadi Dar es Salaam wakitoka kambini Zanzibar na kufanyiwa vipimo.
Kiongera aliingia kwenye mechi dhidi ya Coastal Union kuchukua nafasi ya Amissi Tambwe, lakini akatoka ikiwa imebaki dakika moja na nafasi ya kuchukuliwa na Kiemba ambaye hakugusa hata mpira.

Majeruhi wengine ni Haruna Chanongo ambaye amebakiza siku mbili kabla ya kurudi uwajani na kuanza mazoezi mepesi na Issa Rashid maarufu kama Baba Ubaya.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic