BAHANUZI |
Mshambuliaji Said Bahanuzi ambaye amekuwa hapati
nafasi ya kucheza katika kikosi cha Marcio Maximo, ameifungia Yanga bao pekee
kwenye ushindi wa bao 1-0 dhidi ua timu ya Ambassador FC.
Katika mechi hiyo ya kirafiki mjini Kahama, Ambassador
wanaokipiga daraja la pili ambao ni wenyeji wa Yanga, walikubali kipigo baada
ya Bahanuzi kufunga bao katika dakika ya 41.
Maximo alitumia kikosi chenye wachezaji wengi wanaokaa
benchi ambao walipata nafasi ya kucheza.
Huo ni mchezo wa mwisho kabla ya Yanga kuanza safari
kwenda Bukoba kuivaa Kagera Sugar kwenye Uwanja wa kaitaba mjini Bukoba.
0 COMMENTS:
Post a Comment