Kocha wa Man United, Luis
van Gaal amesema anajua Jose Mourinho wa Chelsea atamuanzisha mshambuliaji Diego
Costa.
Van Gaal ambaye ni kati ya
walimu wa Mourinho amesema tayari wamejiandaa kwa kuwa wanajua Coasta hatakaa
nje licha ya taarifa ya majeruhi ya nyama zake za paja.
Kuonyesha kweli van Gaal
anamjua vizuri Mourinho, taarifa zinasema Costa atakuwa kwenye kikosi cha leo
kwa kuwa jana alifanya mazoezi.
Man United iko ugenini
kuwavaa wagumu hao ambao wamekuwa wakipaa kwenye Premier League na Man United
wanaosua, wanatakiwa kushinda leo ili kuinua hali yao ya kujiamini.
0 COMMENTS:
Post a Comment