Pepe ameamua
kufunguka na kumjibu kiungo mkongwe wa Barcelona, Xavi Hernández aliyesema Real
Madrid hawakuwa na soka la kuvutia zaidi ya ushambulia kwa kushitukiza tu.
Pepe
amesema walirejea kipindi cha pili wakiwa na hamu ya ushindi, wakiwa
wamejiandaa.
“Tulitaka
kushinda na tukafanikiwa kuugeuza mchezo katika kipindi cha pili.
“Tuna
kikosi bora, kushinda Ligi ya Mabingwa si bahati ni uhakika, hivyo anayekutana
na sisi lazima ajue anacheza na timu bora.
“Tunajua
tuna deni na tunatakiwa kufanya kazi yaz iada baada ya hapa,” alisema Pepe
ambaye alifunga bao la pili wakati Real ikiadhibu Barca kwa mabao 3-1 licha ya
kuanza kufunga kupitia Neymar.
0 COMMENTS:
Post a Comment