Kumekuwa na hofu kubwa
kwamba baadhi ya mashabiki wanaokwenda kuangalia mechi kati ya Chelsea dhidi ya
Manchester United, wanaweza kuchelewa.
Imeelezwa mashabiki hao
wanaweza kuchelewa kutokana na njia moja ya treni kuharibika.
Hivyo wakashauriwa kutumia
njia nyingine ya London kwenda katika Uwanja wa Old Trafford.
Walitakiwa wapitie
Sheffield lakini kukawa na hofu ya kuchelewa maana safari itakuwa ndefu kwa
takribani saa mbili na nusu.
Uongozi wa Chelsea umesema
mechi hiyo itachezwa katika muda uliopangwa awali, hivyo hakutakuwa na
mabadiliko na wahusika wakuu ni wenyeji Man United.
0 COMMENTS:
Post a Comment