Kipa Petr Cech wa Chelsea,
ameonyesha kuwa ana vipaji kibao.
Ametupia video kwenye
mtandao wa youtube akipiga drums kwa ubora wa juu kabisa.
Cech alikuwa akipiga na pia
kuimba, hali inayoonyesha ana uwezo wa sanaa na si soka pekee.
Kipa huyo amekuwa akikaa
benchi katika kikosi cha Chelsea, tokea Kocha Jose Mourinho alipoamua
kumrudisha Mbelgiji, Thibaut Courtois aliyekuwa akicheza kwa mkopo katika
kikosi cha Atletico Madrid.
0 COMMENTS:
Post a Comment