Kocha wa Mbeya City, Juma Mwambusi
ameonekana akipiga stori na Hamisi Kiiza wa Yanga.
Mwambusi alifanya hivyo wakati Yanga na
Simba wakipambana kwenye Nani Mtani Jembe kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.
Mazungumzo yao yalionyesha yakisisitiza
jambo huku Kiiza ambaye ametemwa Yanga kumpisha Mliberia, Kpah Sherman
akielezea kitu fulani kwa muda mrefu.
Alipoulizwa Mwambusi kama ilikuwa ni sehemu
ya kumshawishi Mganda huyo kutua Mbeya City, yeye alisisitiza hakuwa yeye.
“Mimi! Sijazungumza na Kiiza labda
umenifananisha,” alisema.
0 COMMENTS:
Post a Comment