January 19, 2015



Klabu ya Arsenal ya Uingereza, ipo kwenye mazungumzo na baadhi ya makampuni ya hapa kwa ajili ya kujenda mahusiano ya kibiashara mbalimbali za vifaa zikiwemo jezi.


Akizungumza na Waandishi wa Habari, Ofisa Biashara wa klabu hiyo, Sam Stone alisema kuwa leo wanatarajia kukutana na makampuni mbalimbali kati ya 20 kwa ajili ya kujadiliana masuala mbalimba ya kibiashara.

Stone alisema, biashara waliyopanga kuifanya ni kuuza jezi zao orijino wanazozitumia kwenye msimu, traki suti, soksi, viatu na vitu vifaa vingine vinavyohusiana na michezo vya Arsenal.

“Tupo hapa nchini kwa ajili ya kujenga mahusiano mazuri ya kibiashara kati ya hapa nchini na klabu ya Arsenal, hivi sasa tupo kwenye mazungumzo na baadhi ya makampuni tutakayofanya nayo kazi pamoja katika kuziuza jezi zetu orijino kwa njia ya mtandano.

“Mpango unaohusisha nchi za Afrika kwa hivi sasa, tulianza na Kenya, Uganda, South Afrika, Nigeria, Misri, Nigeria na hivi sasa Tanzania,”alisema Stone.

    



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic