DOMAYO (KULIA) WAKATI AKIWA YANGA... |
Baada ya kufanikiwa kuing’arisha Azam FC
kwenye mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Stand United juzi, kiungo mahiri Frank
Domayo ametamba kuwa ndiyo anaanza kazi na moto wake utaonekana tu.
Domayo ambaye amerejea hivi karibuni kufuatia
majeraha ya goti yaliyomweka nje kwa takribani miezi saba, alianza kung’aa kwenye
Kombe la Mapinduzi na juzi aliifungia Azam bao pekee lililoipa ushindi dhidi ya
Stand kwenye Uwanja wa Kambarage, Shinyanga.
Domayo alisema kuwa yeye
hapendi kuongea maneno mengi ila ubora wake utazidi kuonekana pindi atakapozidi
kucheza.
“Soka
haliongelewi kwa mdomo, ila ni kwa vitendo pekee, hasa pale unapokuwa uwanjani
uwezo wako ndiyo unaonekana.
“Malengo yangu ni kuhakikisha nafanya vizuri
ili kuibuka mfungaji bora msimu huu, japokuwa nimechelewa kuanza ligi kutokana
na kuwa majeruhi, ila nitahakikisha najitahidi kadiri niwezavyo kurudisha
heshima yangu,” alisema Domayo.
0 COMMENTS:
Post a Comment