January 19, 2015


Tokea alivyoondoka Simba, kocha Mzambia, Patrick Phiri, amekuwa akiichungulia Simba kwa mbali na juzi alitamka kuwa timu hiyo ina nafasi kubwa ya kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu huu kutokana na kikosi kikali ilichonacho.


Hata hivyo, Phiri amesema kuwa ni lazima wachezaji wapambane kutokana na upinzani mkali uliopo kutoka kwa Yanga na Mtibwa Sugar.

Phiri bado hajapata timu ya kufundisha baada ya kuachana na Simba kutokana na matokeo mabaya katika mechi nane za ligi kuu, ambapo timu hiyo ilishinda mchezo mmoja, sare sita na kipigo kimoja. Nafasi yake ilichukuliwa na Mserbia, Goran Kopunovic.

Phiri amesema anaipa Simba nafasi ya kutwaa ubingwa lakini akasisitiza ni lazima ‘wakaze’ buti kwani haiwezi kuwa rahisi kutokana na uwepo wa Yanga na Mtibwa ambazo pia anasema zina nafasi ya kufanya hivyo.

“Ukiniuliza swali hilo nitakwambia timu ninayoijua, Simba wana nafasi ya kuchukua ubigwa msimu huu, kutokana na aina ya wachezaji ilionao. Lakini ni lazima wajitume zaidi maana kuna timu kama Yanga hata pia hao Mtibwa Sugar wana nafasi kubwa ya kuchukua ubingwa,” alisema Phiri.


Simba ya Kopunovic imekuwa moto wa kuotea mbali tangu achukue mikoba hiyo, ambapo umekuwa ni mwendo wa kugawa dozi, wakiwa tayari wamefanya maajabu kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi, ambayo waliondoka na ubingwa kwa kuizima Mtibwa Sugar katika changamoto za mikwaju ya penalti.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic