Mbeya City wameanza tambo kufuatia kushinda
mechi mbili mfululizo kwenye Ligi Kuu Bara.
Uongozi wa timu hiyo ambayo baada ya mapumziko
iliifunga Ndanda bao 1-0 mjini Mbeya, kisha juzi ikaifunga Kagera 1-0 ugenini
kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, umetamka kuwa sasa upo kwenye mikakati ya
kuhakikisha wanamaliza ligi ndani ya nafasi tatu za juu.
Mbeya City ilikwenda mapumziko ikiwa ya mwisho
kwenye msimamo lakini sasa inashika nafasi ya 11.
Msemaji wa
timu hiyo, Dismas Tena, alisema: “Kwa sasa tuna mipango maalumu ya kuhakikisha
tunafanya juhudi za kuweza kurudi katika nafasi tatu za juu kama tulivyofanya msimu
uliopita.
“Na tuna uhakika jambo hilo litatimia kutokana
na ubora wa kikosi tulichonacho ambacho wachezaji wanajituma katika kila mchezo
kuhakikisha tunaibuka na ushindi.”
0 COMMENTS:
Post a Comment