Kinda wa miaka 16 tu,
ameamua kuachana na timu kibao zilizokuwa zikimhitaji na kuamua kutua Real
Madrid.
Kati ya timu zilizokuwa zikimtaka kinda huyo kwa hali na mali ni Manchester United, Manchester City na Liverpool.
Martin Odegaard raia wa
Norway ambaye tayari anaichezea timu ya taifa ya nchi hiyo amejiunga na Real
Madrid kwa kitita cha pauni milioni 2.3. Kinda huyo anaanza kazi huku akilipwa
kitita cha pauni 40,000.
Kijana huyo amesema alikuwa
akivutiwa na mkongwe Zinedine Zidane ambaye amekuwa ushawishi mkubwa sana kwake
kujiunga na Real Madrid.
Martin Odegaard ameonekana
akiwa katika picha ya pamoja na Cristiano Ronaldo na Sergio Ramos baada ya
kuwasili katika mazoezi ya Real Madrid.
0 COMMENTS:
Post a Comment